Personal tools
You are here: Home Books Penzi la Damu

Penzi la Damu

by Anna Manyanza

Mstahamilivu hula mbivu, mtaka cha uvunguni sharti ainame, na mchumia juani hulia kivulini. Ni machache ya maadili yamuongozayo binti Malaika katika safari yake ya kutimiza ndoto zake. Kujiendeleza kielimu ndiyo ndoto yake kuu. Kwa vile Mungu hamtupi mja wake, anabahatika kwenda ughaibuni kitaaluma. Ni safari inayomtenganisha na mpenzi wake, Ben. Lakini Ben anaahidi kumsubiri hadi afuzu masomo yake. Katika kipindi hiki cha utengano, dunia inawapangia mambo mengine kabisa, ni utengano unaotishia kulisumu penzi lao. Majaribu hayeshi, vishawishi ni vingi. Penzi lao linayumba, linatishia kudumbukia kwenye dimbwi la damu. Lakini Malaika haliachii penzi lake kwa Ben, analipigania kishujaa. Ben pia anaingia vitani kulipigania penzi la Malaika. Je, watashinda vita hivi vya kimapenzi?

ISBN 9789987753680 | 154 pages | 229 x 152mm | 2022 | Mkuki na Nyota Publishers, Tanzania | Paperback

Categories:

eBook ISBN: 9789987080182

Authors

Editors

Document Actions